Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akivalishwa skafu mara baada ya kuwasili katika Kituo cha Kumbukumbu na Nyaraka wakati wa ziara ya kikazi na Kamati yake iliyolenga kukagua utekelezaji wa Mradi wa kituo hicho kilichopo Kanda ya Ziwa, Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkoani Mwanza.