Mnakaribishwa kwenye Tovuti ya Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa. Kumbukumbu na... Soma zaidi
Bi. Yunge P. Kanuda, mwakilishi TUGHE Taifa, akitoa rai kwa wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi, kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kutimiza wajibu wao katika kikao cha Baraza la wafanyakazi, kilichofanyika tarehe 06/03/2026
Mkuu wa Kitengo cha Mipango na Tathmini, Bw. Edwin P. Katundu akitoa taarifa ya mwelekeo wa Bajeti ya Idara kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 kwa Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi, katika kikao cha Baraza kilichofanyika tarehe 06/03/2026.
Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi, Bw. Firimin M. Msiangi (kulia) akiteta jambo na Katibu wa Baraza la Wafanyakazi aliyemaliza muda wake, Bw. Pius Mtaki (Kushoto), katika kikao cha Baraza hilo kilichofanyika tarehe 06/03/2026 Dodoma.
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wakifuatilia na kusoma kwa makini Muhtasari na yatokanayo na kikao kilichopita, katika kikao cha Baraza la wafanyakazi kilichofanyika tarehe 06/03/2026, Dodoma
Katibu Msaidizi wa Baraza la Wafanyakazi aliyechaguliwa, Bi. Rose Mtui, akitoa neno la shukrani kwa wajumbe kwa kuchaguliwa kuongoza Baraza. Katibu aliyechaguliwa katika uchaguzi huo ni Bw. Norbert Cyrille (hayupo pichani).
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu Bi. Salama Mohammedi (kushoto) akimsikiliza kwa makini Bi. Happyness Kitalima Katibu wa TUGHE Mkoa (hayupo pichani), alipokuwa akitoa ufafanuzi kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa Katibu na Katibu Msaidizi wa Baraza.
Bi. Happyness Kitalima, Katibu wa TUGHE Mkoa wa Dodoma, ambaye alikuwa ni msimamizi wa uchaguzi wa Katibu na Katibu Msaidizi wa Baraza la Wafanyakazi, akitoa ufafanuzi kabla ya uchaguzi huo kufanyika, tarehe 06/03/2026.
Mkurugenzi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la wafanyakazi, Bw. Firimin M. Msiangi akitoa neno la ukaribisho wakati akifungua kikao cha Baraza, kilichofanyika tarehe 06/03/2026 katika Ukumbi wa mikutano ofisini hapo Dodoma.
Waliomsindikiza Mwalimu kwenye safari yake ya kwanza UNO 1955, kutoka kushoto, Bw. Rashid Sisso, Robert Makange, Iddi Faiz Mafungo, Julius Nyerere, John Rupia, Bibi Titi Mohamed